Job 29:12-17


12 akwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada,
naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.

13 bMtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki,
nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.

14 cNiliivaa haki kama vazi langu;
uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.

15 dNilikuwa macho ya kipofu
na miguu kwa kiwete.

16 eNilikuwa baba kwa mhitaji;
nilimtetea mgeni.

17 fNiliyavunja meno makali ya waovu,
na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.

Copyright information for SwhKC